Millionaire  Ads

Tuesday, March 21, 2017

"Msikubali kuangushwa na wachache, ninyi ni wengi" Hussein Bashe

Tags

March 21, 2017 Mbunge wa Nzega mjini kupitia
CCM Hussein Bashe amepost ujumbe kupitia
ukurasa wake wa Instagram wenye maneno
yaliyosomeka…>>>' Kama taifa wazee wetu
walipoanzisha harakati za kudai uhuru na
hatimaye tukaupata mwaka 1961 walikuwa na
malengo '
' Upo uwezekano mkubwa kwamba sisi viongozi wa
sasa tumewaangusha ninyi raia katika kufikia
malengo ya waasisi wetu ' –Hussein Bashe
' Msikubali kuangushwa na sisi wachache, nyinyi
ni wengi mna mamlaka na nguvu ya kututaka sisi
kuwafikisha kwenye malengo ya Uhuru ' –Hussein
Bashe
' Ni jambo la hatari kwa taifa inapotokea viongozi
wakakosea na kutoka nje ya malengo, wananchi
wakakaa kimya na kuogopa kuonya, kushauri,
kukosoa au hata kukemea sababu tu ya woga au
hofu.'- Hussein Bashe
' Tutakua tunajenga taifa la raia waoga msiingiwe
na woga juu ya kudai haki zenu na kututaka sisi
viongozi kutimiza wajibu wetu ' -Hussein Bashe
' Kwa kushindwa kwenu kutukemea au kutushauri
tunapokengeuka sote tunaingia katika kundi moja
la kuwakosea na kuwasaliti wazee waliopigania
UHURU wa taifa letu. TUJISAHIHISHE ' –Hussein
Bashe

Unaipenda Tanzania acha ujumbe hapa, comment
EmoticonEmoticon