Millionaire  Ads

Monday, November 28, 2016

FIDEL CASTRO AMEFARIKI DUNIA

Tags

Kiongozi wa Kikomunist aliyeongoza chini ya kivuli cha USSR iliyokuwa ikiongozwa na Russia, na Rais Mstaafu wa Cuba, Fidel Castro amefariki dunia, akiwa na umri wa miaka 90, Castro alizaliwa 13th August 1926.

Alimpindua kiongozi aliyekuwa akiungwa mkono na Marekani, Batista mwaka 1959 yeye akiwa kinyume na USA na kuwa upande wa socialists yaani USSR, alishika wadhifa huo wa Urais wa Cuba tangu 1959 mpaka alipojivua gamba na kumuachia mdogo wake Raul Castrol mwaka 2006.

Mazishi rasmi yatafanyika tarehe 04/12/2016 huko nchini Cuba.

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amesema wao wamepoteza rafiki kwani alikuwa upande wao wakati wa kupigania uhuru kutoka kwenye vitendo vya ubaguzi wa Rangi uliokuwa ukiendelea nchini mwao.

Castro alitoa hotuba yake ya nwisho February 2016 ambayo ilibeba wosia ambao kwa maana nyingine ulikuwa ukitabiri kifo chake.

Raul Castro, Rais wa Cuba ametangaza hali ya maombolezo ya Taifa hilo mpaka tarehe 04/12/2016 mazishi ya majivu yake yatakapo fanyika.

Mwandishi:
         Abineri Mwanuke.

Kafulila kuandika kitabu sakata la TEGETA ESCROW

Tags

Aliyewahi kushika wadhifa wa Ubunge na kukaa katika Bunge la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania kupitia chama cha NCCR Mageuzi, David Kafulila amesema yupo mbioni kukitoa kitabu kinachoelezea suala la kashfa ya Tegeteta Escrow.

Hatua hiyo inakuja ikiwa ni Miaka miwili sasa tangu suala hilo kuchukua nafasi kubwa ya majadiliano katika Bunge la Jamhuri.

Kafulila ndiye alikuwa wa kwanza kuliibua suala hilo Bungeni mwaka 2014,
Kashfa ile ilipelekea Mh. Anna Tibaijuka kuachishwa au uteuzi wake wa Uwaziri kutenguliwa na Rais wa awamu ya nne, Mh. Jakaya Mrisho kikwete.

Kafulila anasema yupo katika hatua za mwisho katika kuchapisha kitabu hicho kilichobeba Mengi kuhusiana na sakata la TEGETA ESCROW,
lengo la Kafulila kuandika jambo hilo anasema ni kuweza kuukeza ukweli ili umma ujue kuhusu sakata lile.

Kwasasa sakata hilo halijadiliwi Bungeni lalini TAKUKURU wanasema bado wanaendelea na uchunguzi zaidi ili kuwabaini wahusika wa wizi ule.

Na:
     Abineri Mwanuke.

Wednesday, November 23, 2016

Miundombinu ipewe kipaumbele zaidi, Mikoa mingine waige Morogoro "Msamvu".

Tags

Miundombinu inamchango mkubwa sana kwenye maendeleo ya Nchi yoyote ile duniani.
  Hutumika katika kusafirishia bidhaa na malighafi kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine hata watu pia.
   Miundombinu hii pia hurahisisha shughuli za kibiashara, kwaajili ya miundombinu bei ya bidhaa inaweza ikawa kubwa(kama miundombinu mibovu) na pia bei inaweza ikawa ndogo(kama miundombinu bora)

kwa ujumla miundombinu inarahisisha sana shughuli za uchukuzi au usafirishaji.

   Mkoani Morogoro, manispaa imejikita katika kuboresha kituo kikuu cha Mabasi (Msamvu), wakayi shughuli hiyo ikiwa bado inaendelea lakini tunaweza kusema kwa karibu asilimia 60 wameshafanikisha uboreshaji huo kama inavyoonekana kwenye picha juu.

Hii itakuwa ni chachu ya maendeleo pale mkoani morogoro kwasababu miundo mbinu itakuwa vizuri zaidi ya ilivyokuwa mwanzo, kwasababu hata jinsi ya ukusanyaji wa mapato tunaamini itakuwa imeboreshwa zaidi.

 
Tukija kwenye mikoa mingine kama vile Iringa, Tabora, Kigoma n.k tunaona vituo vya mabasi havijaboreshwa kwa kiwango kizuri kiasi cha kufanya hata shughuli za ukusanyaji mapato kuwa na changamoto zaidi.

   
Japo inawezekana mikoa hiyo nayo pia ikawa kwenye harakati za kufanya mabadiliko au kuboresha miundombinu hasa kwenye vituo vya mabasi na sehemu za kupaki magari ya mizigo, tungewaomba waharakishe sana kwasababu miundombinu ni moja ya chachu ya kukuza sekta nyingine kama vile utalii, kilimo n.k


Imeandikwa na:
           Abineri Mwanuke
  

Monday, November 21, 2016

BULLAYA AZUNGUMZA BAADA YA KUSHINDA KESI YA UBUNGE.

Tags

      Mahakama kuu imetoa hukumu ya kesi iliyofikishwa mahakamani ikipinga ushindi wa Mbunge wa Bunda Ester Bullaya (CHADEMA) dhidi ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Stephen Wasira (CCM) katika uchaguzi uliofanyika October 2015.

  Mahakama hiyo chini ya Jaji Noel Chocha imempa ushindi Ester Bullaya.
kwa maana hiyo Mbunge huyo alishinda kihalali kabisa katika uchaguzi huo.

Baada ya mahakama kutangaza ushindi huo, Bullaya alizungumza:

    "Kiukweli namshukuru sana Mungu na Wananchi wa Jimbo la Bunda Mjini kwasababu walishaamua na Mahakama imeamua lakini kwa uvumilivu wao na hivi ninavyo zungumza kuna watu wametoka Musoma kwa miguu mpaka Bunda wakishangilia ushindi huo"

Kesi hiyo ilifunguliwa mahakamani na wafuasi (wapiga kura) wanne wa Mh. Stephen Wassira.

Sunday, November 20, 2016

BASHE: Lowassa alionewa, kuondolewa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Urais 2015

Tags

Mbunge wa Nzega, Hussen Bashe (CCM), amesema kuondolewa kwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa katika mchakato wa kumpata mgombea wa uraisi kilikuwa ni cha uonevu.

"yaliyo mkuta Lowassa yamewakuta wengi, hilo sio jambo geni. wapo walio amua kuhama chama. CCM ina changamoto hiyo"
alisema Bashe.

Aliongeza, kashfa nyingi katika CCM hutengenezwa, tukikumbuka sakata la Richmond ambalo lilisababisha Edward Lowassa kujiuzulu uwaziri mkuu mwaka 2007, pia sakata la Lugumi na kashfa ya Escrow ambayo haiekeweki imeishia wapi.

kashfa hizo hutengenezwa zikiwa na lengo maalumu aidha kwaajili ya mtu fulani au kikundi cah watu.

Amesema, baada ya Lowassa kuenguliwa katika kinyang'anyiro aliamua kujiunga Chadema lakini kabla ya kuondoka Bashe anasema alijitahidi kumshauri avumilie asihame chama lakini ilishindikana.

pia bashe ameeleza uhusiano wake na lowassa kuwa haupo kabisa kwa sasa.

"Uhusiano wangu na Lowassa ulikuwepo kabla ya yeye kuhamia Chadema lakini kwa sasa sina uhusiano naye wa kisiasa au wa namna nyingine"

amemalizia.

Monday, November 14, 2016

"SITAKI HATA DOLA MOJA YA MSHAHARA WANGU" TRUMP

Tags

Rais mteule wa Marekani Bill. Donald Trump amesema hatachukua hata dola moja ya mshahara wake.

Trump amesema, wakati wa kampeni aliziendesha kampeni zake kwa gharama zake yeye mwenyewe hivyo hata akiwa Rais hahitaji mshahara.

Trump anasemekana kuwa na utajiri wa dola Billion 3.7 ambazo ni sawa na zaidi ya Tsh. Trilioni 8.

      
           By: Abineri Mwanuke

Wednesday, November 9, 2016

ULIPITWA NA HOTUBA YA TRUMP BAADA YA KUSHINDA? ISOME HAPA.

Tags

MAGUFULI AMTUMIA TRUMP SALAMU ZA PONGEZI

Tags

Baada ya vyombo vya habari kuripoti rasmi kuwa Donald Trump ameshinda uchaguzi wa Marekani, Rais wa Tanzania Dr Magufuli amemtumia salamu za pongezi Mh. Trump kupitia Ukurasa wake wa Twitter. 

          "Congratulations President_
          Elect and people of America for
         a democratic election,
         I assure and people of
           Tanzaniafor a continued 
         Friendship"

Imeandikwa na:
            Abineri Mwanuke

BREAKING NEWS : TRUMP AMESHINDA UCHAGUZI WA MAREKANI. CLINTON AKUBALI KUSHINDWA.

Tags

Uchaguzi wa Marekani unaendelea na unakarbia mwisho.

Donald Trump ameshinda baada ya kupata kura 275 dhidi ya 218 za Clinton katika majimbo 45 ambayo yametangaza Matokeo.

pia mshindi alitakiwa kufikia kura 270 tu katika majmbo yote 50.

Clinton naye amekiri kushindwa.

Source: BBC SWAHILI NEWS.

Imeandikwa na:
              Abineri Mwanuke

Tuesday, November 8, 2016

BREAKING NEWS: JOSEPH MUNGAI AFARIKI DUNIA JIONI YA LEO.

Tags

     Waziri wa zamani wa Elimu Tanzania Joseph Mungai amefari dunia jioni ya leo.

chanzo kimeripoti kuwa kabla ya kufariki alitapika mara kadhaa japo haijajulikana chanzo cha tatizo hilo ni nini.

kwa habari zaidi endelea kutufuatilia.

    Imeandikwa na :
                  Abineri Mwanuke

CHADEMA: LEMA APELEKWE MAHAKAMANI.

Tags

    Viongozi Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo (CHADEMA) wamewataka polisi wanao mshikiria Godbless Lema, Mbunge wa Arusha mjini kumpeleka Mbunge huyo mahakamani.

Madai hayo yameyokana na Mbunge huyo kukaa mahabusu kwa muda wa wiki moja, muda ambao wao wamedai ni kinyume cha sheria kwani mtuhumiwa anatakiwa kukaa mahabusu kwa masaa 24 tu na kisha kupelekwa mahakamani.

   Lema anashikiriwa na polisi kwa madai ya kutoa maneno yenye uchochezi.
  hata hivyo kamanda wa polisi Arusha amesema uchunguzi juu ya suala hilo bado unaendelea.

     Imeandikwa na:
                     Abineri  Mwanuke

Monday, November 7, 2016

DODOMA: WABUNGE WA CCM WAJIPANGA KUJIBU TUHUMA ZILIZO TOLEWA NA MBOWE.

Tags

Wabunge wa chama cha mapinduzi wamesema wanatafuta majibu ili kujibu kashfa zilizo tolewa na Mh. Mbowe kwa wabunge wa CCM kwani zinawachafua wao,  cham pamoja na serikali ya Rais Magufuli.

Mbowe alidai kuwa wabunge wa CCM walipewa shilingi milioni kumi (10000000) kila mmoja ili kupitisha Muswada wa habari uliotolewa na Waziri Nape Nnauye.

wanesema msemaji wa chama chao Mh. Olesendeka atatoa kauli au tamko juu ya tuhuma hizo.

      Imeandikwa na:
                 Abineri Mwanuke

BREAKING NEWS: MWENYEKITI MSAIDIZI WA BODI YA LIGI KUU AMEFARIKI DUNIA.

Tags

Saidi Mohammed, makamu mwenyekiti wa bodi ya ligi,  na pia aliyewahi kuwa mwenyekiti wa azam amefariki dunia.

kiongozi huyo amefariki katika hospitali ya Agakhan alikokuwa akipatiwa matibabu.

kwa taarifa zaidi, endelea kutembelea blog hii.

Imeandikwa na:
                  Abineri Mwanuke

Fwd: SIASA ZA MAREKANI, FUNZO KWA TANZANIA (KIDEMOKRASIA).

Tags


---------- Forwarded message ----------
From: "Abineri Mwanuke" <abineri0762@gmail.com>
Date: Nov 7, 2016 4:43 PM
Subject: SIASA ZA MAREKANI, FUNZO KWA TANZANIA (KIDEMOKRASIA).
To: <chatguestforum.tanzania@blogger.com>
Cc:

> no ko Wakati yakiwa yamebakia masaa kadhaa kabla ya uchaguzi wa Marekani kufanyika na kumpata kiongozi wake ambaye kwa upande mwingine anakuwa ni kiongozi Mkubwa sana Duniani, tujifunze machache kidogo ambayo pengine yangeweza kutusaidia watanzania.
>
>     Uwepo wa demokrasia ya kweli kule marekani ni chanzo kikubwa cha amani, mtu anaweza kujiuliza kwanini ninasema ni demokrasia ya kweli... hii ni kwasababu kuna maelewano na makubaliano mazuri kati ya vyama vya upinzani na chama tawala,  wakati huu wa uchaguzi hatujasikia mmarekani yeyote akilalamikia au kuto kuwa na imani na tume ya uchaguzi hii inamaanisha kwamba kwa pande zote mbili wameridhishwa na tume yao tofauti na Tanzania ambayo mwaka jana tumeshuhudia tume ya taifa ya uchaguzi NEC ikilalamikiwa sana kuwa haikuwa ikivitendea haki vyama vya upinzani, hii ni kwasababu hata uundwaji wake si wa kidemokrasia kwani viongozi wake wengi wanaonekana kutokea upande wa chama tawala.
>
>      Uwepo wa midahalo mbalimbali inayowakutanisha wagombea wa Uraisi,  tunaona Donald Trump na Bi Hillary Clinton wamekutana katika midahalo zaidi ya mara 5, ambayo ilikuwa inatoa nafasi kwa kila mmojawapo kumuhoji mwenzie kutokana na kile anachokifanya au alichowahi kukifanya.
>     kwamfano, Bi Clinton alimuuliza Trump kuwa: kwasababu yeye alishawahi kufilisika mara tano katika biashara zake na kuwa assisted (kusaidiwa)  na baba yake, je atawezaje kuingoza marekani kama ana rekodi hiyo,  na kama ikitokea akafilisika atainuaje uchumi wa marekani kwasababu wao ndo taifa kubwa, hakuna wa kumsaidia?....
> pia Trump alipata kumuuliza Clinton kwanini alitumia baruapepe binafsi katika masuala ya kiofisi na Clinton akaweza kujieleza na kuomba msamah kwa hilo.
> Hilo lina panua wigo kwa wananchi kumuelewa zaidi mtu ambaye wangetamani awe kiongozi wao.
> lakini ukiangalia Tanzania mwaka jana haizidi midahalo miwili iliyoandaliwa kwaajili ya wanasiasa ambayo pia wengi wao hawakuhudhuria
>
>         Suala jingine ni Kashfa kwa mtu binafsi, Wamarekani wameendelea zaidi kuliko Nchi yoyote duniani hilo linaeleweka vizuri, masuala ya ufisadi pamoja na rushwa ni nadra sana kuweza kutokea,  ndio maana hata kwa wale wagombea wawili ambao wameshika hatamu katika Uchaguzi wa marekani yaani Donald Trump na Hillary Clinton hakuna ambaye anaonekana kuwa na kashfa za namna hiyo.
>         kwamfano upande wa Donald Trumps amekutwa na kashfa  ya kuwadhalilisha wanawake kwani alionekana akiwa na wanawake ambao walikuwa uchi na akiwafanyia vitu vya aibu miaka ya 1990 (1990's), pia kitendo cha kuwasemea wamarekani weusi maneno mabaya na cha mwisho ni kuvuja kwa picha za uchi za mkewe.
>        Na kwa upande Hillary Clinton ni kuhusiana Kushindwa kutekeleza baadhi ya mambo ambayo wamarekani wengi waliyatarajia kutoka kwake alipo kuwa waziri chini ya Serikali ya Barack Obama na kashfa nyingine zikihusiana na Mumewe Bill Gate Clinton wakati alipokuwa Raisi wa Marekani.
>    mambo yote hayo ukiyaangaliia kwa undani ni masuala binafsi tu yasiyo na uhusiano wowote kisiasa.
>        
>    Upande wa Tanzania vitu vilivyo shika hatamu wakati wa uchaguzi ni ufisadi, Watanzania tunatakiwa kuyaangalia mambo haya na mengine Mengi ya kuigwa kwaajili ya kulinusuru Taifa letu.
> Aidha uhuru unatakiwa kuwepo kwa mamlaka au tume zinazosimamia uchaguzi wa Tanzania Bara na Visiwani yaani ZEC na NEC ili kusiwepo na sintofahamu kwa baadhi ya wanasiasa wakihofia kuibiwa kura au kutotendewa haki katika kipindi cha uchaguzi.
>
> Nna jambo la mwisho ni suala la mfumo wa kupiga kura, Wamarekan wapo vizuri katika mifumo hiyo kwani tunaona mpaka jana tarehe 06.11.2016 zaidi y wamarekani million 42 walikuwa wamekwisha kupiga kura, japo siku rasmi kabisa ni kesho tarehe 08.11.2016 lakini wanamfumo ambao unaruhusu kupiga kura siku saba kabla ya siku ya uchaguzi.
> hii inasaidia kwanza kupunguza msongamano wa watu siku ya zoezi rasmi lakini pia Inasaidia mtu kuwa na uhuru wa kupiga kura huku mabo mengine yakiendelea vizuri.
>
> Lakini kwa mfumo huu wa Tanzania, bado kuna changamoto kubwa kwasababu watu wengi wanashindwa kufanya maamuzi/kpiga kura kwasababu ratiba inakuwa inabana kwasababu siku ya uchaguzi ni moja na hat mtu akiwa nje ya jimbo lake haruhusiwi kupiga kura, hii inapoteza ukweli wa demokrasia kwani demokrasia ya kweli ni ile inayohusiaha uchaguzi wa haki na uhuru.
>      
>      Watanzania tubadilike kwasababu tunakuwa kama bado hatuna uhuru, yaani tupo chini ya wakoloni tusiowaona ambao wanaweza kuwa ni, Ujinga na Umasikini, tupige hatua kubwa kuwang'oa hawa ili nasisi tuwe angalau na Demokrasia ya Ukweli na Uwazi.

Imeandikwa na:
Abineri Mwanuke

SIASA ZA MAREKANI, FUNZO KWA TANZANIA (KIDEMOKRASIA).

Tags

no ko Wakati yakiwa yamebakia masaa kadhaa kabla ya uchaguzi wa Marekani kufanyika na kumpata kiongozi wake ambaye kwa upande mwingine anakuwa ni kiongozi Mkubwa sana Duniani, tujifunze machache kidogo ambayo pengine yangeweza kutusaidia watanzania.

    Uwepo wa demokrasia ya kweli kule marekani ni chanzo kikubwa cha amani, mtu anaweza kujiuliza kwanini ninasema ni demokrasia ya kweli... hii ni kwasababu kuna maelewano na makubaliano mazuri kati ya vyama vya upinzani na chama tawala,  wakati huu wa uchaguzi hatujasikia mmarekani yeyote akilalamikia au kuto kuwa na imani na tume ya uchaguzi hii inamaanisha kwamba kwa pande zote mbili wameridhishwa na tume yao tofauti na Tanzania ambayo mwaka jana tumeshuhudia tume ya taifa ya uchaguzi NEC ikilalamikiwa sana kuwa haikuwa ikivitendea haki vyama vya upinzani, hii ni kwasababu hata uundwaji wake si wa kidemokrasia kwani viongozi wake wengi wanaonekana kutokea upande wa chama tawala.

     Uwepo wa midahalo mbalimbali inayowakutanisha wagombea wa Uraisi,  tunaona Donald Trump na Bi Hillary Clinton wamekutana katika midahalo zaidi ya mara 5, ambayo ilikuwa inatoa nafasi kwa kila mmojawapo kumuhoji mwenzie kutokana na kile anachokifanya au alichowahi kukifanya.
    kwamfano, Bi Clinton alimuuliza Trump kuwa: kwasababu yeye alishawahi kufilisika mara tano katika biashara zake na kuwa assisted (kusaidiwa)  na baba yake, je atawezaje kuingoza marekani kama ana rekodi hiyo,  na kama ikitokea akafilisika atainuaje uchumi wa marekani kwasababu wao ndo taifa kubwa, hakuna wa kumsaidia?....
pia Trump alipata kumuuliza Clinton kwanini alitumia baruapepe binafsi katika masuala ya kiofisi na Clinton akaweza kujieleza na kuomba msamah kwa hilo.
Hilo lina panua wigo kwa wananchi kumuelewa zaidi mtu ambaye wangetamani awe kiongozi wao.
lakini ukiangalia Tanzania mwaka jana haizidi midahalo miwili iliyoandaliwa kwaajili ya wanasiasa ambayo pia wengi wao hawakuhudhuria

        Suala jingine ni Kashfa kwa mtu binafsi, Wamarekani wameendelea zaidi kuliko Nchi yoyote duniani hilo linaeleweka vizuri, masuala ya ufisadi pamoja na rushwa ni nadra sana kuweza kutokea,  ndio maana hata kwa wale wagombea wawili ambao wameshika hatamu katika Uchaguzi wa marekani yaani Donald Trump na Hillary Clinton hakuna ambaye anaonekana kuwa na kashfa za namna hiyo.
        kwamfano upande wa Donald Trumps amekutwa na kashfa  ya kuwadhalilisha wanawake kwani alionekana akiwa na wanawake ambao walikuwa uchi na akiwafanyia vitu vya aibu miaka ya 1990 (1990's), pia kitendo cha kuwasemea wamarekani weusi maneno mabaya na cha mwisho ni kuvuja kwa picha za uchi za mkewe.
       Na kwa upande Hillary Clinton ni kuhusiana Kushindwa kutekeleza baadhi ya mambo ambayo wamarekani wengi waliyatarajia kutoka kwake alipo kuwa waziri chini ya Serikali ya Barack Obama na kashfa nyingine zikihusiana na Mumewe Bill Gate Clinton wakati alipokuwa Raisi wa Marekani.
   mambo yote hayo ukiyaangaliia kwa undani ni masuala binafsi tu yasiyo na uhusiano wowote kisiasa.
       
   Upande wa Tanzania vitu vilivyo shika hatamu wakati wa uchaguzi ni ufisadi, Watanzania tunatakiwa kuyaangalia mambo haya na mengine Mengi ya kuigwa kwaajili ya kulinusuru Taifa letu.
Aidha uhuru unatakiwa kuwepo kwa mamlaka au tume zinazosimamia uchaguzi wa Tanzania Bara na Visiwani yaani ZEC na NEC ili kusiwepo na sintofahamu kwa baadhi ya wanasiasa wakihofia kuibiwa kura au kutotendewa haki katika kipindi cha uchaguzi.

Nna jambo la mwisho ni suala la mfumo wa kupiga kura, Wamarekan wapo vizuri katika mifumo hiyo kwani tunaona mpaka jana tarehe 06.11.2016 zaidi y wamarekani million 42 walikuwa wamekwisha kupiga kura, japo siku rasmi kabisa ni kesho tarehe 08.11.2016 lakini wanamfumo ambao unaruhusu kupiga kura siku saba kabla ya siku ya uchaguzi.
hii inasaidia kwanza kupunguza msongamano wa watu siku ya zoezi rasmi lakini pia Inasaidia mtu kuwa na uhuru wa kupiga kura huku mabo mengine yakiendelea vizuri.

Lakini kwa mfumo huu wa Tanzania, bado kuna changamoto kubwa kwasababu watu wengi wanashindwa kufanya maamuzi/kpiga kura kwasababu ratiba inakuwa inabana kwasababu siku ya uchaguzi ni moja na hat mtu akiwa nje ya jimbo lake haruhusiwi kupiga kura, hii inapoteza ukweli wa demokrasia kwani demokrasia ya kweli ni ile inayohusiaha uchaguzi wa haki na uhuru.
     
     Watanzania tubadilike kwasababu tunakuwa kama bado hatuna uhuru, yaani tupo chini ya wakoloni tusiowaona ambao wanaweza kuwa ni, Ujinga na Umasikini, tupige hatua kubwa kuwang'oa hawa ili nasisi tuwe angalau na Demokrasia ya Ukweli na Uwazi.

Tangazo kwa mwandishi wa blog hii

Tags
Habari ndugu mwandishi, Hongera kwa kuanza kuandika blog hii ili ulipwe. Tunataka tukupe maelekezo zaidi ya kutambua malipo.

Tunaomba mwisho wa makala yako uandike mfano Imeandikwa na Anna tesha  

TANZIA: SAMUEL SITTA AFARIKI DUNIA.

Tags

Aliyewahi kuwa spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania na waziri wa Uchukuzi mstaafu, Mh. Samuel Sitta amefariki dunia alfajiri ya leo huko nchini Ujerumani alikokuwa akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa mtoto wa hayati S. Sitta, Benjamin Sitta amesema baba yake alipelekwa huko nchini ujeruman Alhamisi kutokana na kuwa na saratani ya tezi dume ambayo ilitembea mpaka miguuni na kuathiri mwili mzima.

Mh. Sitta amefariki akiwa na umri wa miaka 74.

Enzi za uhai wake, amelitumikia taifa katika nyanja mbalimbali ikiwemo kuwa Spika wa Bunge (2005-2010) akiwa pia Mbunge wa Urambo.
pia Mh. Samuel Sitta alikuwa ni mmoja ya wagombea 42 waliochukua fomu za kuwania kupewa ridhaa na CCM kugombea Urais wa Tanzania mwaka 2015.
Bwana ametoa Bwana ametwaa, jina lake libarikiwe.
AMINA.